Monday 25 May 2015

Jeshurun's Mind: Kiswahili na Mashairi


KANILEMAZA

Mwenzenu kanilemaza, na kunivaa moyoni,
Mengi yamenipendeza, siulize kwa nini,
Mengine ni miujiza, ameshushiwa mwandani.

Ukweli haufichiki, kajaaliwa imani,
Undani yeye hataki, penye kosa hubaini,
Umbile hamithiliki, bashasha za kila fani.

Mkweli kakamilia, anafahamu hisani,
Mpole zake tabia, si mtu wa ushindani,
Mzuri katimilia, aloazimu amini.

Anajua nampenda, moyoni ameamini,
Ameridhi kuniganda, katu hatubandukani,
Popote ninapokwenda, yumo mwangu mawazoni.

Mtunzi: Sihaba Juma